Mshambuliaji wa kimataifa Thomas Emmanuel Ulimwengu amesema kwamba kwa
sasa pengo la Mtanzania mwenzake, Mbwana Ally Samatta linaonekana TP
Mazembe.
Ulimwengu akiongea na Clouds FM alisema TP Mazembe kwa sasa inamkosa mshambuliaji mwepesi, mwenye uwezo wa kufunga kama Samatta.
Samatta ameondoka timu hiyo ya DRC Januari mwaka huu baada ya kushinda
nayo taji la Ligi ya Mabingwa Afrika na kujiunga na KRC Genk ya Ubelgiji
anakoendelea vizuri hivi sasa.
Tangu kuondoka kwa Samatta, Mazembe imeonekana kupoteza makali yake kiasi cha kuvuliwa mapema ubingwa wa Afrika.
Mazembe ilitolewa na Wydad Casablanca ya Morocco katika hatua ya 16 Bora
ya Ligi ya Mabingwa na kuangukia kwenye kombe la Shirikisho.
Katika mechi iliyopita Mazembe ilipata ushindi mwembamba wa bao 1-0
katika mchezo wa kwanza wa mchujo kuwania kuingia hatua ya makundi ya
Kombe la Shirikisho la Soka Afrika dhidi ya Stade Gabesien Uwanja wa
Mazembe mjini Lubumbashi.
Ulimwengu aliyecheza kwa dakika 45 juzi kabla ya kutoka uwanjani akiwa
anachechemea, alisema timu kwa sasa haina mtaalamu wa kufunga mabao kama
alivyokuwa Samatta.
“Pengo la Samatta linaanza kuonekana sasa, pale mbele hakuna na
anayeweza kufunga kama Samatta, tunapoteza nafasi nyingi sana, hilo
ndilo tatizo,”amesema Ulimwengu.
Sasa Mazembe itakuwa na kazi ngumu katika mchezo wa marudiano wiki
ijayo, ikitakiwa kwenda kuulinda ushindi huo mwembamba nchini Tunisia
News
Wednesday, May 11, 2016
0 Response to "Thomas Ulimwengu Afunguka Pengo la Samatta bado lipo TP Mazembe"
Post a Comment