Obama: UK kupoteza ushawishi wake ikijiondoa EU

blogger templates

                     Image caption Rais Obama na waziri Mkuu wa Uingereza Cameron

Rais wa Marekani Barack Obama amasisitiza kuwa Uingereza itapoteza ukuaji na ushawisi wake iwapo itaamua kuondoka katika muungano wa Ulaya kupitia kwa kura ya maoni mwezi Juni.
Akiongea baada ya mazungumzo na waziri mkuu wa Uingereza David Cameron mjini London, Obama alisema kuwa Uingereza itakuwa nyuma katika kuafikiana mikataba ya kibiashara na Marekani ikiwa itaondoka.
Wale wanaounga mkono kuondoka kwa Uingereza wamekosoa hatua za rais Obama za kuingilia kati suala hilo.
Obama hatahivyo amesema kuwa hakuwa na nia ya kushawishi kura bali kuongea ukweli kama rafiki

0 Response to "Obama: UK kupoteza ushawishi wake ikijiondoa EU"

Post a Comment