Ripoti: Jay Z Kuja na Album yake Atakayousema Ukweli Wake Kama Alivyofanya Beyonce Kwenye Lemonade

blogger templates
Jay Z analikamua limao lake mwenyewe pia.
Mtu wa karibu na familia hiyo, ameliambia jarida la US Weekly kuwa rapper huyo, 46, anarekodi nyimbo zitakazoeleza upande wake wa kilichotokea kwenye ndoa yake na Beyonce.

April 23, Queen Bey, 34, aliwashangaza mashabiki kwa video maalum iliyorushwa na HBO pamoja na album ya Lemonade, inayoelezea tetesi za muda mrefu za kusalitiwa na mume wake kwa mashairi kama: This is your final warning / You know I give you life / If you try this s‑‑t again / You gon’ lose your wife.”

Watu wanadai kuwa wawili hao walikuwa mbioni kuachana kabisa mwaka 2014 baada ya tukio maarufu kwenye lifti. May 2014, TMZ walivujisha video inayomuonesha mdogo wake Beyoncé, Solange Knowles, akimshambulia Jay Z wakiwa kwenye lifti baada ya kuhudhuria hafla ya Met Gala.

Vyanzo vinadai kuwa wanandoa hao waliweza kumaliza tofauti zao na sasa wako imara tena.

0 Response to "Ripoti: Jay Z Kuja na Album yake Atakayousema Ukweli Wake Kama Alivyofanya Beyonce Kwenye Lemonade"

Post a Comment