Rais Magufuli Asema yeye Siyo Katili, Anawatumikia Watanzania ili Kurejesha nchi Kwenye Mstari

blogger templates
Rais John Magufuli amewataka Watanzania wasimuone katili kwa kuwafukuza kazi baadhi ya watendaji wa Serikali, kwakuwa anataka kuirejesha nchi kwenye mstari.

Akizungumza katika misa ya Jumapili kwenye Kanisa Katoliki Parokia ya Tokeo la Bwana Burka jijini Arusha, Rais Magufuli alisema watu katili ni wale ambao walikuwa wanawaibia Watanzania na kuwanyonya wanyonge.

Dk Magufuli alisema analazimika kuchukua hatua ya kuwafukuza kazi si kwamba ni katili, bali lengo ni kuwatumikia Watanzania na kuirejesha nchi kwenye mstari.

Alisema Tanzania ni taifa tajiri, hakuna sababu ya wananchi kulalamika kila kona, kwani kuna ardhi ya kutosha, madini ya kila aina, wanyama wa aina mbalimbali ambao baadhi wameanza hadi kupelekwa nje.

“Ninapochukua hatua nataka kuweka Tanzania iliyonyooka, mimi tayari nimesema nimejitoa sadaka kwa Watanzania hasa wanyonge,” alisema.

Aliongeza kuwa hatawaangusha Watanzania na hatabadilika, ataendelea kusimama na kutetea haki za Watanzania maskini na siku zote atatembea na maskini.

0 Response to " Rais Magufuli Asema yeye Siyo Katili, Anawatumikia Watanzania ili Kurejesha nchi Kwenye Mstari"

Post a Comment