Mtoto mwenye umri wa miaka 10 nchini Finland amewashangaza watu wengi
baada ya kugundua udhaifu katika mtandao wa kijamii wa Instagram.
Mvulana huyo kwa jina Jani ametunukiwa $10,000 (£7,000) baada ya
kugundua udhaifu huo uliowezesha mtu kuingia kwenye mtandao huo wa
kusambaza picha na kufuta maoni ya watu.
Jambo la kushangaza zaidi ni kwamba kisheria haruhusiwi kutumia mtandao
huo hadi atimize umri wa miaka 13. Kampuni ya Facebook ambayo inamiliki
Instagram, ilichukua hatua upesi na kuondoa udhaifu huo.
Sasa, ndiye mtu mchanga zaidi kutunukiwa pesa kwa kugundua udhaifu
katika mitandao ya kampuni hiyo. Aliandikia wasimamizi wa mtandao huo
barua pepe Februari kuwafahamisha kuhusu ugunduzi wake.
Wataalamu wa mtandao huo walimfungulia akaunti ndipo aweze kuthibitisha
madai yake na akafanikiwa. Mvulana huyo kutoka Helsinki, ameambia gazeti
la Iltalehti la Finland kwamba atatumia pesa hizo kununua baiskeli,
mpira na mavazi ya kuchezea kandanda na kompyuta za kutumiwa na ndugu
zake.
Facebook imeambia BBC kwamba imelipa jumla ya $4.3m kwa watu waliogundua
udhaifu kwenye mitandao yake. Malipo hayo hutolewa kama kishawishi
kuzuia watu kuuzia wahalifu ugunduzi wao na hivyo kusaidia kampuni
husika.
News
Wednesday, May 4, 2016
0 Response to "Huu ni Udhaifu wa Instagram Uliogunduliwa na Mtoto wa Miaka 10"
Post a Comment