SABABU ZA MWANAUME KUSHINDWA KURUDIA ‘TENDO

blogger templates

 

 



Inashauriwa kwa mwanawake kusitisha kwa muda purukushani za huba pindi atakapobaini kuwa mwenza wake anavuta kasi ya kuongeza gia. Isitoshe dondoo za mazungumzo zinashauriwa sana kuchukua nafasi, isiwe ni kasi kwa kwenda mbele kana kwamba mapenzi ni mchezo wa kukomoana au ni pambano la kumpata mshindi.

Mapenzi hayako hivyo na sio lazima yafanyike kwa mhemko mkali kwa kipindi chote kana kwamba ni mbio za mita mia.

Pamoja na hayo wanawake wanashauriwa kutoa angalizo la umbali wao katika kufikia kilele ili kumpa fursa mwanaume naye kupata kipimo cha wakati wa kumaliza. Angalizo hilo litamsaidia kumfanya apoteze mawazo kwa hofu ya kuonekana hafai kwa kitendo cha kumwacha mwenzake njia panda.

Kusema kweli hili sio tatizo kubwa linalohitaji tiba ya matatibu kwa kiasi hiki, isipokuwa ni kupata elimu ya kutambua uwezo wa miili yetu.

Kwa maana hiyo maelezo ya dondoo zifuatazo yanaweza kumsaidia mwenye tatizo hili.

MAZOEA YA MWILI: Watu wengi wenye majukumu hujikuta wakiizoeza miili yao kwa kufanya mapenzi kwa tendo moja kutokana na kukosa nafasi, kwao kukutana na mwanamke kwa maana hiyo miili yao hukosa hamasa ya kurudia kutokana na mazoea. Hivyo muhusika anapotaka kwenda raundi nne lazima aanze kuuzoeza mwili kidogo kidogo asifikiri atakurupuka mara moja na kwenda mara tano.

UMRI WA MTU: Kuna baadhi ya wanaume wengine wa ajabu sana; wanajikuta wakihangaika kutafuta dawa za nguvu za kiume eti kwa sababu hawaendi kama zamani ilhali wanajua fika nguvu za mwili hupungua kutokana na umri unavyokwenda.

HAMASA KUSHUKA: Upofu mwingine wa kimawazo ni kwa wanaume na wanawake kutotambua kuwa hamasa ya kimapenzi hushuka kulingana na muda wa
wapendanao kuwa pamoja. Kuna wengine wanadhani kuwa watadumu kwenda mara sita au saba kama walivyokuwa wakati wa uchanga wa penzi lao.

Katika hili wanapaswa kutambua siku zote mwili wa mwanadamu una desturi ya kuzoea kile ambacho kinafanyika kila siku. Kwa mfano kama wewe huna desturi ya kunywa chai asubuhi, mwili wako hauwezi kudai chakula hicho kamwe kutokana na kwamba sivyo ulivyozoezwa.

Lakini kama mwili huohuo utazoezwa kinyume chake na kulishwa chai kila asubuhi basi itakuwa vigumu kwa mhusika kupitisha masaa hayo kama hakutia kinywaji hicho mdomoni. Hivyo basi kabla ya kwenda hospitali au kubwia madawa ya kuongeza nguvu jiulize maswali juu ya mazoea yako.

Na kama ukitaka kubadilisha mazoea hayo kumbuka kuwa haitakuwa jambo la leo bali litachukua muda kuliwekea kumbukumbu katika mwili wako.

Hivyo basi nawashauri wale wote ambao wanashindwa kurudia kufanya tendo wafanye utafiti juu ya nini kinapungua katika ushindwaji wao.

Lakini pia wasikubali kukata tamaa na kujiona hawawezi eti kwa sababu wamekutana na mwanamke fulani na wameshindwa kufanya hivyo.

0 Response to "SABABU ZA MWANAUME KUSHINDWA KURUDIA ‘TENDO"

Post a Comment