Inashauriwa kwa mwanawake kusitisha kwa
muda purukushani za huba pindi atakapobaini kuwa mwenza wake anavuta
kasi ya kuongeza gia. Isitoshe dondoo za mazungumzo zinashauriwa sana
kuchukua nafasi, isiwe ni kasi kwa kwenda mbele kana kwamba mapenzi ni
mchezo wa kukomoana au ni pambano la kumpata mshindi.
Mapenzi hayako hivyo na sio lazima yafanyike kwa mhemko mkali kwa kipindi chote kana kwamba ni mbio za mita mia.
Pamoja na hayo wanawake wanashauriwa
kutoa angalizo la umbali wao katika kufikia kilele ili kumpa fursa
mwanaume naye kupata kipimo cha wakati wa kumaliza. Angalizo hilo
litamsaidia kumfanya apoteze mawazo kwa hofu ya kuonekana hafai kwa
kitendo cha kumwacha mwenzake njia panda.
Kusema kweli hili sio tatizo kubwa
linalohitaji tiba ya matatibu kwa kiasi hiki, isipokuwa ni kupata elimu
ya kutambua uwezo wa miili yetu.
Kwa maana hiyo maelezo ya dondoo zifuatazo yanaweza kumsaidia mwenye tatizo hili.
MAZOEA YA MWILI:
Watu wengi wenye majukumu hujikuta wakiizoeza miili yao kwa kufanya
mapenzi kwa tendo moja kutokana na kukosa nafasi, kwao kukutana na
mwanamke kwa maana hiyo miili yao hukosa hamasa ya kurudia kutokana na
mazoea. Hivyo muhusika anapotaka kwenda raundi nne lazima aanze kuuzoeza
mwili kidogo kidogo asifikiri atakurupuka mara moja na kwenda mara
tano.
UMRI WA MTU:
Kuna baadhi ya wanaume wengine wa ajabu sana; wanajikuta
wakihangaika kutafuta dawa za nguvu za kiume eti kwa sababu hawaendi
kama zamani ilhali wanajua fika nguvu za mwili hupungua kutokana na
umri unavyokwenda.
HAMASA KUSHUKA: Upofu mwingine wa kimawazo ni kwa wanaume na wanawake kutotambua kuwa hamasa ya kimapenzi hushuka kulingana na muda wa
wapendanao kuwa pamoja. Kuna wengine wanadhani kuwa watadumu kwenda mara
sita au saba kama walivyokuwa wakati wa uchanga wa penzi lao.
Katika hili wanapaswa kutambua siku zote
mwili wa mwanadamu una desturi ya kuzoea kile ambacho kinafanyika kila
siku. Kwa mfano kama wewe huna desturi ya kunywa chai asubuhi, mwili
wako hauwezi kudai chakula hicho kamwe kutokana na kwamba sivyo
ulivyozoezwa.
Lakini kama mwili huohuo utazoezwa
kinyume chake na kulishwa chai kila asubuhi basi itakuwa vigumu kwa
mhusika kupitisha masaa hayo kama hakutia kinywaji hicho mdomoni. Hivyo
basi kabla ya kwenda hospitali au kubwia madawa ya kuongeza nguvu
jiulize maswali juu ya mazoea yako.
Na kama ukitaka kubadilisha mazoea hayo
kumbuka kuwa haitakuwa jambo la leo bali litachukua muda kuliwekea
kumbukumbu katika mwili wako.
Hivyo basi nawashauri wale wote ambao
wanashindwa kurudia kufanya tendo wafanye utafiti juu ya nini kinapungua
katika ushindwaji wao.
Lakini pia wasikubali kukata tamaa na
kujiona hawawezi eti kwa sababu wamekutana na mwanamke fulani na
wameshindwa kufanya hivyo.
0 Response to "SABABU ZA MWANAUME KUSHINDWA KURUDIA ‘TENDO"
Post a Comment